Hello! Maswali Yako yote yamejibiwa😊

1. Mbona Video Kwangu haziplay– Kama video kwako haiplay jaribu kubadilisha mtandao, Au kuwasha VPN.

2. Jinsi ya kuondoa Pop up ya “Tazama Tangazo“- Shughuli zetu pia zinaendeshwa Kwa Gharama kubwa tu hivyo tunajitahidi kuhandle gharama hizo Kwa wewe kuangalia Tangazo. Kuondoa hio pop up, kwanza bonyeza neno Tazama Tangazo na utatolewa nje ya app na kupelekwa kwenye browser Yako kule ambapo tangazo lipo. Wewe itakubidi ufatishe tangazo linachohitaji kama kubonyeza button zake zote utakazo ziona. Ukishavuta sekunde kadhaa unaweza Rudi kwenye app na kuendelea kufurahia content Yako.

3.Nashindwa Kudownload Movie SwahiliPlay na Nikisearch Movie Sizipati– Kama unapitia changamoto hio tafadhali bonyeza hii LINK ukajifunze jinsi ya kusearch na kudownload movie bila shida

4. Mbona magame yanauzwa na sio Bure– Magame hayo mengi ni mod na watu kama wewe Ndio kazi zao ambapo hukesha hata mwaka mzima kuliunda, kulitoa game Hilo Bure ni kama tunawakatisha tamaa wazalishaji hao hivyo sisi tutakuuzia Kwa bei ya chini.

5. Mbona SpeedPlay haifanyi kazi– Wenda Server ziko kwenye Maboresho, hivyo vuta subra

🤩Kama unashida nyingine tofauti, I comment hapo chini, itatolewa ufafanuzi ndani ya masaa 12🤩

Leave your comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

50 Comments

  1. Ahh inazingua sanaaa Yani Kila ukitaka kuplay kitu inakwmbia katazame tangazo na Fanya unchoambiwa lkn unenda mbaka mwsh na ukiludi mambo ndo Yale Yale Yani Inazngua Sanaa alafu mbaya zaid tangazo unakuta hata halieleweki linataka nn Yani dah munakata stimu kinoma Yani😡

    1. utakua unajaribu kulog in kama mtu mwenye account ndo maana ina kataa, kwenye hilo eneo la ku log in angalia kwa chini utaona neno register, ulibonyeze ndo utafungua account

  2. Kuna movie zingine ukizifungua ukitaka kudawnload haina ile option hiyo kwann unakuta tu open link tena hizi movie mpya. Na ukirudi nyuma kwenye page kama ulikuwa kwenye movie ya mbele basi unarudi nyuuma kabisa kiukweli hiii app ina boa kama vp mui update ikae sawa

      1. Feedbacks kutoka kwa walaji wako ni nzuri kwa huduma bora. Hasa kwa mtu ambaye ana ndoto kubwa kwenye ulimwengu wa teknolojia. Ukipewa maoni ukawa unayachukulia poa na kujibu watu kama hawana msaada kwako si kujenga. Kumbuka mnategemeana, wewe unahisi unaweza kupata pesa unayopata kupitia matangazo bila watu kufungua hii WEBSITE au APP Yako? YOU NEED TO BE POSITIVE. Kwanini usimueleweshe vyema, kwa maana hicho alichokisema kwamba baadhi ya muvi hazina download option ni kweli.. Na baadhi kila ukitaka kuzipakua zinaandika download failed. UMEFANYA KAZI NZURI, BUT INATAKIWA UWE CHANYA.

        1. Ni kweli kabisa kiongozi uko sahihi, customer care inahitajika sana ili sote tuzidi kuendelea kupeana support, sote tunategemeana. Lakini hata kama kuna mapungufu katika app hii au website, Sisi watumiaji tujitahidi kuuliza kwa utaratibu bila kutumia lugha ya hasira wala matusi kwa sababu tujue kuwa tunawasiliana na binadamu na sio app wala website. Kwani ubora na maboresho yanategemea maoni ya wadau wa app na website hii.

    1. Pia kuna changamoto ambayo naipitia kwa sasa tangu jana, nikiwa na download muvi inakuwa haifiki mwisho naambiwa download failed kwenye hii website Yako. Shida inawezakuwa ni nini? Kwa maana nikitaka kupakua vitu vingine vinavyopatikana nje ya website hii vina downloadika tena very fast.

      1. Unaambiwa download failed na nani? The moment ukipress download button, na ikaanza kudownload, Huyo ni simu yako na sio sisi tena! Kutatua changamoto hio jaribu kutumia website na sio App ili vitu unavyo vidownload viwe vinajilist kwenye browser yako

  3. Habari. Ni kwanini Movie nyingi ambazo ni mpya yaani zilizotafasiriwa hivi karibuni hazina option ya kudownload? Option zilizopo ni Watch live, Link, Subscribe, Rate.
    MAONI: Ni vyema app hii pamoja na website zifanyiwe maboresho katika kipengele cha history. Ili hata ukiwa katika movie au page ya 5 ukirudi nyuma iweze kurudi kwenye page ya 4,3,2,1 kisha menyu kuu. Na sio ikurudishe moja kwa moja kutoka page ya 5 hadi menyu kuu.
    Ahsanteni.

  4. Sanahan broo nilikua naulizia kama nitapata squid-game- season 2 ambayo imetafsiriwa kiswahili maana si wengine tulikimbia shule.. au kama itashindikana Kuna plan B ya kupata subtitles ya kiswahili kama inawezekana nielekeze

  5. Na mm inanizingua nikitaka kuplay kitu inahama tovuti inaingia phonex sasa mi nataka ukiingia naingia au nikiplay naplay video bc

  6. Nahitaji kujua jinsi ya kujitoa na hii huduma kwani inajilipa yenyewe baada ya mara ya kwanza kuingiza namba yangu ya siri imekuja kulipia tena huduma hata wiki mbili haijapita tena bila mm kuruhusu hivyo itakua inaniibia hela zangu.

      1. kwanza nikupe ongera sana SwahiliPlay sababu hii kazi uliyo fanya sio kazi rahisi kweli unafaa kupata watu wengi wa download app yako au wa tembeleye website yako, alafu unafanya haya yote kwa bure kabisa. acha niseme ahsante kwa niamba ya watu wengine. Thank you.

  7. Nimefungua hii app lakin chaajabu! Zimekuja tu movie pamoja na mechi 1 ya mpira, isitoshe naplay hiyo mechi yenyew ya bayern munchen na sttutgat lakin haiplay bali inakataa tu zinaonesha movie tu. Tatizo nini??

  8. Tatizo langu kubwa nikwamba mbona kila nikijaribu ku click mfano Live videos and movie au Mpira tv Live badala ifunguke hiyo inakupeleka moja kwa moja kwenye betway ili kuanza kubashiri michezo wakati mi sina mood ya kucheza kamali